Sunday, August 13, 2017

THE NATIONAL COUNCIL FOR TECHNICAL EDUCATION

 (NACTE)

 TAARIFA KWA UMMA

KUHUSU KUHAMA KWA OFISI YA NACTE KANDA YA KASKAZINI

Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE), linapenda kuuhabarisha Umma na wadau wa Elimu nchini hasa wa kanda ya Kaskazini ya kwamba, ofisi ya baraza ya kanda ya kaskazini imehamia katika jengo jipya la NSSF COMMERCIAL COMPLEX (MAFAO HOUSE) ghorofa ya nane (8), jengo hili lipo katika barabara ya Old Moshi, Plot No. 1. Karibu na New Arusha Hotel kuelekea Kibo Palace Hotel.

Kabla ya kuhama ofisi hizo zilikuwa katika majengo ya Arusha Technical College (ATC) Chumba namba nne (4), karibu na njia panda ya barabara ya kuelekea Nairobi (Namanga Road) na ile inayotoka Moshi.

Kwa maelezo zaidi, wasiliana na Ofisi zetu za Kanda ya Kaskazini kwa anuani zifuatazo;-

NACTE Northern Zone
P.o. Box 14333 Arusha,
Mobile: 0658444556/57


IMETOLEWA NA;
KITENGO CHA HABARI MAWASILIANO
BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI (NACTE)
3/08/2017

No comments:

Post a Comment