Friday, August 11, 2017

2 MPANGO MKAKATI WA HAKIELIMU 2017 – 2021 (MUHTASARI)
Dondoo muhimu kuhusu HakiElimu
HakiElimu ilianzishwa mwaka 2001 na kundi la Watanzania 13 ambao waliweka nia thabiti na dhamira ya
dhati na ya muda mrefu kuleta mabadiliko kwenye elimu ya umma kwa watoto wote.
Dira
Kuwa na Tanzania yenye uwazi, haki na demokrasia ambapo watu wote wanafurahia haki ya kupata elimu
bora inayokuza usawa, ubunifu na kufikiri kiyakinifu.
Dhamira
Kuwawezesha watu kubadilisha elimu, ndani na nje ya shule; kushawishi utungaji wa sera na utekelezaji
wenye ufanisi; kuchochea mijadala bunifu ya umma na mabadiliko ya kijamii; kufanya tafiti, uchambuzi wa
sera na utetezi na kushirikiana na wadau ili kukuza ushiriki wa wananchi, uwajibikaji, uwazi na haki za kijamii.

No comments:

Post a Comment