Tuesday, November 28, 2017

District councils unite for Gender Sensitive Budgets.

TGNP Mtandao hosted a two days experience sharing session with District chairpersons and mayors from Tarime, Ilala, Kishapu, Morogoro Rural and Mbeya districts as part of exchanging information and strategies on how to develop gender sensitive budgets.
As part of learning, TGNP Mtandao introduced the officials on various gender concepts and key areas that will be more potential when developing a gender sensitive budget, including water, health, agriculture and education.
Speaking during the session, Chairperson of Kishapu district, Mr Boniface Butondo explains on how gender budgeting has solved the problem of girls missing school during the menstruation days due to lack of facilities to cater them in schools such as Sanitary pads and clean water.
“ On our 2017/2018 budget we are fortunate to provide 30 Million as part of helping young girls who cannot afford sanitary pads in school, that has assisted them to attend school without missing, before we had this money, girls used to miss out 3 to 5 days because they lacked such facilities“ He explained.

 Chairperson of Kishapu district, Mr Boniface Butondo speaking during the session at TGNP Mtandao premises at Mabibo, Dsm
Recalling during the 2017 Gender festival, TGNP awarded the districts that managed to include the issue of sanitary pads to girls in schools that being Kishapu district and Kisarawe. This motivated various districts councils to take such step. This was proven by Mr Moses Misiwa Chairperson of Tarime District.
“ I am very excited attend this session, personally i was very inspired by my fellow district councils as we witnessed them awarded by the Vice president during the Gender Festival. As part of learning i would like to promise that this issue of sanitary pads will be included in our budgets, and am confident to say that we can afford that from our district revenues“ he says.
Apart from menstrual hygiene to girls in schools, the district chairpersons have also complained urging TGNP Mtandao to use the same force to address issues around agriculture. Recently the sector has been left behind by the government and it affects women who are the main actors.
Putting aside their political parties affiliations, the councils from the two districts agreed to set fund from internal sources to ensure that their budgets are very gender sensitive.
” we agree it is inevitable to develop if we are no being fair to some groups in the communities mostly women” they all say. 

Monday, November 27, 2017

Je unazijua siku 16 za kupinga ukatili wa Kijinsia?

Siku 16 za kupinga ukatili wa Kijinsia ni kampeni  ya Kimataifa  inayoongozwa na Kituo cha Kimataifa cha wanawake katika uongozi tangu mwaka 1991. Chimbuko la 16 za kupinga unyanyasaji wa kijinsia na mauaji ya kinyama ya kina dada wa Mirabelle yaliyofanyika nchini Dominica mwaka 1960. Mwaka 1991 Umoja wa Mataifa (UN) ulichagua Novemba 25 iwe siku ya Kimataifa ya Kupinga Ukatili wa Kijinsia ambapo kilele chake huadhimishwa Desemba 10 ya kila mwaka.
Siku hizi 16 hutoa mwanga wa uelewa kwa jamii kwa siku nyingine muhimu kama Novemba 29 ambapo ni siku ya Kimataifa ya watetezi wa haki za Wanawake , Desemba 1,Siku ya Ukimwi Duniani, Desemba 6 siku ya mauaji ya kikatili ya Montreal 1989 (wanawake 14 waliuawa na mtu aliyekuwa anawachukia wanawake) na Desemba 10 siku ya Haki za Binadamu Duniani.
Lengo la maadhimisho haya ni kutoa fursa kwa wanawake, wanaume,Vijana wa kike na kiume na wanaharakati wengine kukuza uelewa wa umma juu ya mchango wa wanawake katika maendeleo na kutafakari matokeo ya harakati za ukombozi wa mwanamke Kimapinduzi sambamba na kutafakari mafanikio hayo kwa miaka 20 ya tangu kuanzishwa kwa harakati hizo nchini mwaka 1993 TGNP ilipoanza.
Tutakumbuka kuwa maadhimisho haya huanza Novemba 25, ambayo ni siku ya Kimataifa ya Kupinga Ukatili dhidi ya Wanawake hadi Desemba 10 ambayo ni Siku ya Haki za Binadamu Ulimwenguni.  Siku hizi 16, TGNP na mashirika mengine yanayotetea haki, usawa wa Kijinsia na ulinzi dhidi ya makundi yaliyoko pambezoni hasa wanawake  wanaadhimisha kwa kufanya shughuli mbalimbali za kijamii, ikiwepo kusikiliza visa mkasa, kutoa shuhuda hadharani, kushirikina na mamlaka za kiserikali na dola latika kuunganisha nguvu kutokomeza kabisa Uakatili wa Kijinsia

Thursday, November 23, 2017

Vumilia,
Secondary scholar,
Tanzania

At just 13-years-old, Vumilia had supported herself through primary school, earning money collecting and selling firewood. But after completing primary school, she despaired in the knowledge that she could not progress to secondary school. Like many families, the cost of uniforms, books, shoes and school fees were beyond Vumilia’s parents’ means. And, to make matters worse, the nearest school was 10km away.  

Her grandmother said that Vumilia felt helpless, refusing to eat and crying every day. “She would ask me ‘Why is there no one to support me?’ I could only say, ‘You see how our life is. We cannot afford your school fees.’” All Vumilia could do was wait.
Before becoming a boarder, Vumilia started her 10 km walk to school at 4.30 a.m. every dayVumilia used to start her 10 km walk to school at 4.30 a.m. every day
Vumilia and her classmates complete forms identifying their school needs to CamfedVumilia and her classmates complete forms identifying their school needs to Camfed
After weeks of anxiety, and at her grandmother’s urging, Vumilia left home at 4:30 a.m. and began the long journey to secondary school. She had no uniform, no stationery, no pencils and no ability to pay her school fees. She had only the love of learning, and a hope that someone could help. When she arrived, she was crying and scared. Fortunately, the local secondary school is a Camfed partner school. Upon learning of Vumilia’s struggles, the head of the school provided her with a uniform, shoes and supplies from Camfed, allowing her to start school that very day. A week later, Vumilia was also invited to stay at the school’s makeshift dormitory space, where 140 other girls were also lodging to avoid long daily walks to school.
Upon learning that Vumilia would be supported through school, and would no longer have to endure the long daily walks, her grandmother was overjoyed. “We are very grateful,” she said. “She won’t live like this anymore.”

CHINA NA TANZANIA KUENDELEA KUSHIRIKIANA KATIKA SEKTA YA ELIMU.

Jamhuri ya Watu wa China imesema itaendela kuisaidia Tanzania katika sekta ya Elimu kwenye eneo la Elimu ya Juu, utoaji wa mafunzo ya Ufundi pamoja na kusaidia garama za uchapishaji wa vitabu vya masomo ya Sayansi kwa ajili ya shule za msingi na Sekondari.
Kauli hiyo imetolewa na Balozi wa wa Jamuhuri ya watu wa China Wang Ke wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako katika ofisi ndogo zilizopo jijini Dar es Saalam.
Katika mazungumzo yao Waziri Ndalichako amesema gharama za uchapaji wa Vitabu ni kubwa hivyo ni vyema Wizara ikawa na mitambo yake ya kuchapia vitabu ambayo itakuwa endelevu suala ambalo Balozi Wang Ke amekubaliana nalo na kuitaka Wizara kuandaa maombi ya mashine hiyo ili ubalozi uweze kufanyia kazi.
Jamhuri ya Watu wa China imesema itaendela kuisaidia Tanzania katika sekta ya Elimu kwenye eneo la Elimu ya Juu, utoaji wa mafunzo ya Ufundi pamoja na kusaidia garama za uchapishaji wa vitabu vya masomo ya Sayansi kwa ajili ya shule za msingi na Sekondari.
Kauli hiyo imetolewa na Balozi wa wa Jamuhuri ya watu wa China Wang Ke wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako katika ofisi ndogo zilizopo jijini Dar es Saalam.
Katika mazungumzo yao Waziri Ndalichako amesema gharama za uchapaji wa Vitabu ni kubwa hivyo ni vyema Wizara ikawa na mitambo yake ya kuchapia vitabu ambayo itakuwa endelevu suala ambalo Balozi Wang Ke amekubaliana nalo na kuitaka Wizara kuandaa maombi ya mashine hiyo ili ubalozi uweze kufanyia kazi.

UCHIMBAJI VISIMA HALMASHAURI YA NSIMBO

HALMASHAURI NCHINI ZA SHAURIWA KUBUNI VYA VIPYA VYA MAPATOI

Halmashauri nchini zimeshauriwa kubuni vyanzo vipya vya mapato ili ziweze kupata mapato ambayo yatasaidia katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo katika ngazi ya serikali za mitaa. Hayo yamesemwa Oktoba 27, 2017 mjini Dodoma na wawakilishi wa idara mbalimbali za Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) wakati wa mkutano uliojumuisha wanachama wa Policy Forum (PF) na maafisa wa OR-TAMISEMI.
Mkutano huo ulikuwa na lengo la kukutanisha wanachama wa PF na maafisa wa idara za OR-TAMISEMI kujadiliana namna ya kufanya kazi kwa pamoja hasa katika sekta ambazo zinaweza kuleta mabadiliko katika ngazi ya serikali za mitaa.
Mkutano huo ulitanguliwa na utambulisho wa pande zote mbili ambapo upande wa PF, Mwenyekiti wa Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa (LGWG), Kellen Mngoya alitoa usuli kuhusiana na mtandao wa PF na kazi zinazofanywa na vikundi kazi viwili ambavyo ni Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa (LGWG) na Kikundi Kazi cha Bajeti (BWG). Utambulisho wa OR-TAMISEMI ulitolewa na Sebastian Kitiku ambaye ni Mratibu wa Idara TAMISEMI.
Kitiku alianza kwa kutoa utangulizi wa jinsi ambavyo OR-TAMISEMI ilivyoalikwa kwenye mkutano wa wanachama wa PF wa  robo mwaka uliofanyika 2016 na kuomba wanachama wa PF kutumia maarifa na ujuzi wao katika kurahisisha miongozo iliyoandaliwa na OR-TAMISEMI kwa ajili ya matumizi katika ngazi za Serikali za Mitaa nchini.
Kitiku alipongeza juhudi zilizoonyeshwa na wanachama wa PF hasa wa kikundi kazi cha LGWG kwa kuweza kurahisisha miongozo hiyo kuwa katika lugha rahisi. Alitaja miongozo hiyo kuwa ni:
  • Mfumo wa Ruzuku ya Maendeleo ya Serikali za Mitaa: Mwongozo wa Ufuatiliaji na Tathmini;
  • Mfumo wa Ruzuku ya Maendeleo ya Serikali za Mitaa: Mwongozo wa Upimaji wa Mwaka na
  • Mfumo wa Ruzuku ya Maendeleo ya Serikali za Mitaa: Mwongozo wa Utekelezaji na Uendeshaji.
Wajumbe wa kikao hicho pia walipata nafasi ya kuweza kujadili suala la Serikali Kuu kuchukua baadhi ya vyanzo vya mapato vilivyokuwa vinakusanywa na Halmashauri. Akitolea ufafanuzi juu ya suala hilo Kitiku alieleza kuwa Serikali Kuu iliamua Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ikusanye kodi katika vyanzo vya mapato vya Serikali za Mitaa kwa kuwa ilionekana Halmashauri hazikuwa na mifumo madhubuti ya kukusanya mapato. Hata hivyo alieleza kuwa zoezi hilo ni la majaribio tu na linafanywa kwenye Halmashauri 30 ambazo ni kubwa ili kupima ufanisi katika ukusanyaji wa mapato.
Kitiku alieleza kuwa kwa sasa Serikali ina mpango wa kuboresha upelekaji wa fedha katika ngazi za Halmashauri. Mpango huo umeainishwa vyema katika vitabu vilivyoandaliwa na OR-TAMISEMI na kuandikwa kwa lugha rahisi na kikundi kazi cha PF na vitazinduliwa Oktoba 28, 2017 mjini Dodoma.
Wajumbe wa mkutano huo waliitimisha majadiliano kwa kukubaliana kuwa bado kuna umuhimu mkubwa wa kuwa na Hati ya Makubaliano (MoU) baina ya PF na OR-TAMISEMI. Pia OR-TAMISEMI iliiomba PF iwapatie watumishi wake mafunzo ya Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) ili waweze kutekeleza vyema shughuli zao za usimamizi wa utekelezaji wa SDGs katika ngazi za mikoa na mitaa.
Pia ilipendekezwa kuwa kikundi kazi cha LGWG kiwe kinashirikiana na Idara ya Serikali za Mitaa ya OR-TAMISEMI hasa katika kazi zinazohusiana na mafunzo kwa madiwani au uchambuzi wa sera mbalimbali zinazohusu Serikali za Mitaa, hili lilikuwa pia ni pendekezo litakalohitajika kuonekana kwenye Hati ya Makubaliano. Wajumbe walikubaliana pia kuwa wakati kikundi kazi cha LGWG kikiwa kinatembelea Halmashauri kiwe kinaenda na angalau afisa mmoja kutoka OR-TAMISEMI.

Friday, October 20, 2017

Baraza la mitihani Tanzania yatangazoa mataokeo ya mtihani wa darasa la saba uliofanyika mwezi septemba mwaka huu Mkoa wa Katavi bado unaendelea kuwepo kwenye oradha ya Mikoa 10 bora kwani umeshika nafasi ya 9 kwa kuwa na Wilaya mbili ambazo ni Mpanda ikishika nafasi ya 9 na Wilaya ya Mlele ikishikanafasi ya 6 kwa pamoja tuwapongeze walimu na wadau mbalimbali walioweza kushiriki kwa namna moja au nyingine kufanikisha ufaulu huo.

Thursday, September 28, 2017

  
Mageuzi ya mifumo kandamizi kwa usawa wa kijinsia na Maendeleo Endelevu”
Tamasha la Jinsia la 14 linahitimishwa leo, Tarehe 8 Septemba 2017, baada ya siku nne za sherehe, tafakuri, mijadala na pongezi. Tamasha lilizinduliwa kwa hotuba ya kusisimua na yenye busara nyingi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan. Pia, Makamu wa Rais alijumuika nasi katika kuwatambua, kuwasherehekea na kuwaenzi  wanawake walioonyesha ujasiri katika Harakati za Ukombozi wa Mwanamke Kimapinduzi, na Halmashauri za Wilaya za Kishapu na Kisarawe ambazo zimefanya vizuri katika kuingiza masuala ya kijinsia katika bajeti za halmashauri zao. Wanawake waliopata tuzo ni pamoja na Mhe. Makamu wa Rais mwenyewe, Mhe.   Mama Getrude Mongella, Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Anna Makinda, Profesa Daktari Mama Esther Mwaikambo, Mhe. Mama Anna Abdalla na Mhe.  Dada Esther Bulaya, Mbunge Bunda Mjini. Wengine ni  Wanachama wa TGNP  Mtandao  waliotoa mchango mkubwa  katika kujenga  Tapo  la Ukombozi  wa wanawake  kimapinduzi akiwemo  Dada  Profesa Marjorie Mbilinyi, Asseny Muro, Mary Rusimbi, Demere Kitunga, Subira Kibiga , Aggripina Mosha na   Zippora Shekilango
Tamasha la mwaka huu, limehudhuriwa na washiriki zaidi ya 1500 wakiwakilisha AZAKI mbalimbali, Vikundi vya kijamii, Serikali, Taasisi za Elimu ya Juu, Wadau wa Maendeleo, Taasisi za Vijana, vyama vya siasa, viongozi mbalimbali na watu binafsi kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani.
Katika Tamasha, siku ya pili na ya tatu kumekuwa na warsha mbalimbali (nane) na mijadala ya kina juu ya haki ya kiuchumi kwa wanawake na rasilimali kuwanufaisha wanawake na wanaume walioko pembezoni. Pia tumejadili uwekezaji wa rasilimali ili kuendeleza usawa wa kijinsia, upatikanaji wa huduma za jamii, na ukatili wa kijinsia  na namna unavyoathiri ushiriki wa wanawake katika maendeleo. Kulikuwa na ushiriki mkubwa wa kimkakati wa vijana hususan wa kike ili kukuza mijadala kati ya rika moja na lingine.
Katika warsha na mijadala hiyo, washiriki waliibua masuala kadhaa na kutoa mapendekezo ya nini kifanyike ili kupata suluhisho la changamoto na vikwazo kwa wananchi.  Kwa Ujumla washiriki  waliona  kuwa pamoja na kutambua na kusherehekea mafanikio  ya ushiriki uliotukuka wa wanawake katika michakato mbalimbali ya kuleta usawa wa jinsia na Maendeleo, bado kuna changamoto  hususan za kimifumo ambazo  zinaminya  fursa za wanawake  kushiriki kikamilifu  katika Maendeleo. Mifumo ya Kiunchumi bado haijaweza kumkomboa  mwanamke hasa wale masikini na wa vijijini. Mifumo ya kisiasa nayo bado ina changamoto katika kutoa fursa sawa za ushiriki wa wanawake katika ngazi za maamuzi  katika nyanja zote. Zaidi mifumo ya kijamii  hususan ufikiaji wa huduma za kijamii bado inazidi kuwaongezea wanawake mzigo wa majukumu huku wakisukumwa  kwa kiasi kikubwa katika sekta isiyo rasmi.
Yafuatayo ni baadhi ya masuala yaliyoibuliwa:
  1. Utengwaji wa rasilimali bado ni changamoto hasa katika kukuza na kuendeleza usawa wa kijinsia na kuwawezesha wanawake. Kwa mfano, ni asilimia 20 tu ya wanawake Tanzania wanamiliki ardhi. Kumekuwa na ufinyu wa rasilimali zinazotengwa kwa ajili ya asasi za kiraia na vikundi vya kijamii hasa hasa rasilimali fedha, ujuzi, teknolojia na taarifa sahihi. Na hii imesababishwa na utegemezi kwa wafadhili kwa kiwango kikubwa. Kwa upande wa serikali, licha ya juhudi zinazofanyika, ikiwemo kutenga asilimia 10 ya fedha za serikali za mitaa kwa ajili ya wanawake na vijana, bado kuna changamoto ya taarifa sahihi juu ya nani ananufaika nazo na nini kifanyike kuboresha hali hiyo. Aidha, hakuna mfumo mzuri wenye uwazi na endelevu wa ufuatiliaji wa rasilimali na utoaji wa mrejesho.
  2. Mfumo wa kukusanya takwimu, kama vile za umiliki wa ardhi, una mapungufu mengi. Zoezi hili linatakiwa kufanyika kwa umakini zaidi ili kuonesha mgawanyo wa umiliki wa ardhi wa wanawake, ukatili wa kijinsia na mimba za utotoni – ili lisaidie katika kutatua changamoto.
  3. Uwekezaji katika sekta ya kilimo – wa pembejeo, maafisa ugani, masoko – uende sambamba na hali halisi ya uzalishaji ili kuboresha maisha ya wananchi na kuchangia ipasavyo katika Tanzania ya viwanda.
  4. Sera mbalimbali za kumwezesha mwanamke na kuinua usawa wa kijinsia haziendani na mazingira ya sasa. Kwa mfano, mitaala ya elimu iliyopo haiendani na sera ya kuelekeza Tanzania kwenye viwanda na uchumi wa kati. Sera zifanyiwe marejeo ili ziendane na muktadha wa sasa, na ziwe na mrengo wa kijinsia. Pia, ziendane na miongozo na mikakati mbalimbali ya kitaifa na kimataifa kama vile malengo ya maendeleo endelevu, Ajenda ya Afrika 2063, Mkataba wa Jinsia na Maendeleo wa SADC, mpango wa maendeleo wa miaka mitano na mpango wa taifa wa kutokomeza ukatili wa kijinsia.
  5. Bajeti kuu na bajeti za serikali za mitaa zizingatie mahitaji ya kijinsia kwa makundi yote. Bajeti iwe ya kutekelezeka, itolewe kwa wakati na kwa kiwango kilichopangwa. Vile vile, mchakato wa kuandaa bajeti uwe shirikishi na wa uwazi, bila kujali tofauti za kijiografia, rika, hali ya uchumi, jinsi, elimu na hali ya ulemavu. Washiriki wa Tamasha tumeazimia kuweka nguvu za pamoja katika kufanya uchambuzi na kufuatilia mchakato wa bajeti na kutoa mrejesho na mapendekezo ya kuboresha mipango na bajeti za serikali katika  ngazi ya Jamii  hadi taifa.
  6. Tanzania ya viwanda na kuelekea uchumi wa kati inahitaji nguvu kazi yenye afya bora na weledi. Hivyo basi, mikakati ya kupunguza vifo vya kina mama na watoto ni muhimu. Hivi sasa watoto 67 kati ya vizazi hai 1,000, na wanawake 556 kati ya 100,000 wanakufa kutokana na huduma duni za afya ya uzazi. Bajeti ya afya iongezwe kufikia asilimia 15 ya bajeti ya taifa, kama  Azimio la Abuja linavyotamka. Pia wananchi watambue wanajukumu  la kufuatilia na kutoa taarifa za vifo na kudai uwajibikaji kwa wahusika.
  7. Upatikanaji wa maji safi na salama bado ni changamoto kubwa, wanawake bado wanatembea kati ya saa tatu hadi tano kutafuta maji. Pia, ukosefu wa maji shuleni na katika vituo vya afya  na zahanati ni changamoto nzito sana. Hii husababisha wanawake wajawazito kubeba ndoo za maji wakati wa kwenda kujifungua, na watoto wa kike kukosa masomo ya siku 40 hadi 50 kwa mwaka wakati wa hedhi. Hivyo, wanafunzi hao hukosa haki yao ya msingi ya masomo na kufaulu vizuri.  Vile vile, maendeleo ya viwanda yatahitaji maji zaidi ili kuwezesha uzalishaji.  Haya yote yataongeza mahitaji ya maji kwa kiwango kikubwa, na hivyo kusababisha ushindani wa uhitaji wa maji kati ya binadamu, mifugo na viwanda, ambapo waathirika wakuu watakuwa ni wanawake.
  8. Mimba za utotoni zimeendelea kuwa changamoto na kikwazo kikubwa sana cha wasichana kupata haki yao ya elimu. Kwa mujibu wa Idara ya Maendeleo ya Vijana – Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu, mimba za utotoni nchini zimeongezeka kutoka asilimia 23 mwaka 2010 hadi kufikia asilimia 27 mwaka 2016/17, kutokana na ukosefu wa huduma ikiwemo  elimu ya afya ya uzazi kwa vijana wenye umri kuanzia miaka 15 hadi 19.
  9. Kuna mapungufu makubwa katika utunzanji wa kumbukumbu, hasa za wanawake wanaochangia katika maendeleo ya taifa, licha ya kwamba wanawake wanachangia maendeleo bega kwa bega na wanaume lakini kumbukumbu zao hazijaandikwa. Na ndio maana katika Tamasha hili, kufuatia utafiti wetu mdogo, TGNP ILITOA TUZO kwa baadhi ya wanawake hao kama sehemu ya kutambua michango yao, na sehemu ya mipango endelevu ya kurithisha ujuzi na maarifa kwa vizazi vipya pamoja na kujifunza kwa wanawake na wanaume waliobobea katika nyanja maalum.
Mikakati
  • Kushirikisha wadau mbalimbli zikiwemo AZAKI, wadau wa maendeleo, asasi za elimu ya juu na taasisi za serikali katika kutafuta na kufanya uchambuzi ili kupata taarifa na takwimu sahihi juu ya mimba na ndoa za utotoni, ukatili wa kijinsia  na umiliki wa ardhi kwa wanawake na watu wenye ulemavu.
  • Kuendelea kuimarisha mikakati ya kuweka kumbukumbu za wanawake waliotoa michango katika maendeleo kwenye nyanja mbalimbali na kuzisambaza taarifa za kumbukumbu hizo kwa ajili ya watu kujifunza na kuwaenzi wanawake hao. Pia, kupanua wigo wa kutoa mafunzo ya kimwongozo katika kuchukua na kuhifadhi kumbukumbu za wanawake kwa AZAKI, vijana na wadau wengine.
  • Kuweka mipango endelevu ya kurithisha ujuzi na maarifa kutoka kizazi/rika moja kwenda nyingine, hasa kutoka kwa wanawake waliobobea kwenye tasnia mbalimbali.
  • Zaidi ya 60% ya Watanzania wakiwa vijana, sera na mipango iingize masuala ya vijana ili waweze kushiriki kikamilifu katika maendeleo katika nyanja zote. Pia, rasilimali za kutosha zitengwe ili kuwezesha utekelezwaji wa mipango na mikakati ya vijana bila kujali itikadi, jinsi, dini, jiografia na hali ya kipato.
By Tumaini Msowoya, Mwananchi tmsowoya@mwananchi.co.tz
Dar es Salaam. Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) imesema mkoa wa Katavi ndio unaoongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya wasichana wanaopata mimba wakiwa na umri mdogo.
Akizungumza kwenye maadhimisho ya siku ya idadi ya watu duniani, Mkurugenzi wa NBS Albina Chuwa alisema takwimu zinaonyesha mkoa huo unaongoza kwa asilimia 36.8, Tabora 36.5 na Simiyu 32.1 huku Dar es Salaam ukiwa mwishoni kwa asilimia 12.
kwa mujibu wa takwimu kutoka Shirika la watu duniani (UNFPA), Tanzania ni miongoni mwa nchi tatu zinazoongoza kwa tatizo hilo barani Afrika.
Kutokana na hali hiyo, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto , Ummy Mwalimu aliitaja jamii kutoendeleza vitendo vya udhalilishaji kwa watoto wa kike, huku akidai kuwa lazima hatua za haraka za kukabiliana na tatizo hilo zifanywe.
Awali Mkurugenzi wa huduma za afya wa Shirika la Maria Stopes, Dk Joseph Komwihangiro alisema  ili kupambana na hali hiyo lazima wasichana wapewe elimu kuhusu masuala ya uzazi ili waweze kujilinda na ndoa za utotoni.
Takwimu zinaonyesha zaidi ya asilimia 10 ya wasichana walio na umri mdogo wameanza kutumia njia za uzazi wa mpango.
Mwisho.

ELIMU BURE






ImageImage
Statement by Tanzania Education Network (Ten/Met) on violence against students in schools
Share Tweet
Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE
Member organizations of Tanzania Education Network (TEN/MET)[1] with deep concern condemn the recent violence against a student perpetrated to Sebastian Chingulu a form three student at Mbeya Secondary School, Mbeya region.
We at TEN/MET commend the Government through the Ministry of Education, Ministry of Reginal Administration and Local Government and Ministry of Home Affairs for taking immediate actions in addressing the situation; including legal actions against the school’s Head Teacher and the involved teachers-on-training for their brutal actions contrary to the rules guiding  administration of corporal punishment in schools.
This is just one incident which has been brought to public attention through various media. The question is, how many incidents as such occur in schools and pass without public knowledge?
While supporting the statements released by different stakeholders condemning the incident, TEN/MET would solely focus on systems of teacher education and student care and development which if strengthened, reduce such actions or incidents.
In fact, the issue brings up a lot of questions regarding teacher education system in Tanzania. The first concern is on the selection of students intending to study teaching. It is possible that the report on the character of the students selected to join teaching is not considered. For example, previously, teachers of the given school could propose a course that a student should take (self-form) considering many factors including student’s character. As a result, students with not teaching character end up joining teaching courses thus get involved such incidents as occurred in Mbeya.
Secondly, it is possible that the teaching curriculum emphasizes more on how to teach than student’s nurturing and development, teacher’s ethics as well as code of conduct that guide the relationship between teachers and students. Thirdly, it shows that there is a management problem at Mbeya Secondary School after failing to take measures in line with the laws and regulations guiding administration of corporal punishment which stipulates that a student can be canned not more than 4 strokes administered by the School Head or any other person delegated by the School Head.
Recommendations:
  1. Students selected to join teaching profession should be recommended by their former secondary schools (form four/six) after character assessment.
  2. The teaching curriculum used to teach  in Universities’ should be reviewed with  proper incorporation of key components pertaining students behavior nurturing, teachers ethics as well as code of conduct guiding the relationship between teachers and students.
  3. Student corporal punishment guideline should be distributed to all colleges offering teaching courses for the purpose of circulating among students.
  4. The government should set up a formal system of reporting incidents of violence against students.
  5. The teaching environment in schools should be friendly to both female and male students.
  6. Teachers’ union (CWT) at all levels should set up a regular routine of training teachers in order to build friendly relationship with students.
  7. Students should respect their teachers and incase of concerns, proper reporting should be done including informing parents/guardians, Head of School or School Board.
  8. Parents should make follow up on their children’s educational and discipline progress and also nurture  children’s discipline and respect towards their teachers.
Released by
Coordinator, TEN/MET

[1] Tanzania Education Network/Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET) is a national education network of 170 Civil Society Organizations (CSOs) working in the education sector in Tanzania.

Sunday, August 13, 2017

THE NATIONAL COUNCIL FOR TECHNICAL EDUCATION

 (NACTE)

 TAARIFA KWA UMMA

KUHUSU KUHAMA KWA OFISI YA NACTE KANDA YA KASKAZINI

Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE), linapenda kuuhabarisha Umma na wadau wa Elimu nchini hasa wa kanda ya Kaskazini ya kwamba, ofisi ya baraza ya kanda ya kaskazini imehamia katika jengo jipya la NSSF COMMERCIAL COMPLEX (MAFAO HOUSE) ghorofa ya nane (8), jengo hili lipo katika barabara ya Old Moshi, Plot No. 1. Karibu na New Arusha Hotel kuelekea Kibo Palace Hotel.

Kabla ya kuhama ofisi hizo zilikuwa katika majengo ya Arusha Technical College (ATC) Chumba namba nne (4), karibu na njia panda ya barabara ya kuelekea Nairobi (Namanga Road) na ile inayotoka Moshi.

Kwa maelezo zaidi, wasiliana na Ofisi zetu za Kanda ya Kaskazini kwa anuani zifuatazo;-

NACTE Northern Zone
P.o. Box 14333 Arusha,
Mobile: 0658444556/57


IMETOLEWA NA;
KITENGO CHA HABARI MAWASILIANO
BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI (NACTE)
3/08/2017

Tamko la HakiElimu juu ya Sera Mpya ya Elimu ya 2014

JOHN KALAGE MKURUGENZI MTENDAJI  HAKI ELIMU
Ndugu Wananchi; Itakumbukwa kwamba Februari 13, 2015 Sera Mpya ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 ilizinduliwa na aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete. Sera hii inaanza kutumika Mwaka huu (2016) wa masomo.
Sera hii, imefuta na kubatilisha matumizi ya sera nyingine za elimu zilizokuwa zikitumika kabla ya Mwaka 2015, zikiwamo Sera ya Elimu na Mafunzo (1995), Sera ya Elimu ya Ufundi na Mafunzo (1996), Sera ya Taifa ya Elimu ya Juu (1999) na Sera ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano kwa ElimuMsingi (2007).
Lengo la Sera hii, linatajwa kuwa ni kushughulikia changamoto za ki-elimu ambazo zinajitokeza zikiwemo udhaifu katika mfumo wa elimu na mafunzo, uhaba wa walimu, uhaba wa zana, nyenzo na vifaa na miundombinu ya kufundishia na kujifunzia pamoja na changamoto katika ithibati na udhibiti wa ubora wa shule na vyuo katika ujumla wake ambavyo vimechangia katika kushuka kwa ubora wa elimu na mafunzo nchini.
Ili kufanikisha lengo hilo, Sera imependekeza hatua mbalimbali ikiwamo kupunguza miaka ya kupata elimu kutoka 18 (2+7+4+2+3+) hadi 16 (1+6+4+2+3); Kiswahili na Kiingereza kuwa lugha za kufundishia katika ngazi zote, kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia na kutoa ElimuMsingi bila Ada sambamba na kupunguza michango ya wazazi shuleni.
Ndugu Wananchi; tukiwa miongoni mwa wadau muhimu katika kuhakikisha maendeleo ya elimu nchini, HakiElimu kama shirika ambalo linataka kuona elimu nchini ikiwa bora, yenye usawa na yenye kuwajengea uwezo wahitimu kukabiliana na changamoto za kimaisha na ushindani katika soko, tumepitia tumetathmini malengo na mapendekezo yaliyomo ndani ya Sera hiyo, na tungependa kutoa maoni au msimamo wa shirika kuhusu Sera hii mpya kama ifuatavyo:
Kuhusu ubora wa elimu
Pamoja na kuwa malengo ya sera yanataja kuhakikisha kuwa elimu inayotolewa nchini inakuwa bora na ya viwango vya ushindani, sera imeshindwa kufafanua ni jinsi gani itahakikisha kuwepo kwa ubora huo. Katika uchambuzi tumeonesha kuwa tafiti nyingi zinakubali kuwa ili elimu inayotolewa iwe yenye ubora ni lazima taifa lijitahidi kuboresha mazingira ya ufundishaji na kuwekeza katika ubora wa walimu ambao ndio msingi wa elimu yenyewe.
Hata hivyo Sera hii imekuwa kimya juu ya suala la ubora wa walimu na mazingira yao ya kuishi na kufanyia kazi. Sera haitamki suala la kuboresha maslahi ya mwalimu.
Aidha, ili kuhakikisha ubora mashuleni, shule, taasisi na vyuo vinapaswa kufanyiwa ukaguzi kuhusu ufundishaji, ujifunzaji, mazingira n.k. Hata hivyo sera hii haitoi mwongozo maalumu kuhusu namna ubora wa elimu utakavyo tathiminiwa na jinsi ya kuimarisha ukaguzi. Itakumbukwa kuwa Idara ya Ukaguzi kwa kipindi kirefu imekuwa ikikabiliwa na changamoto lukuki zikiwemo za uhaba wa bajeti na wataalamu. Takwimu zinaonesha kuwa hali ya ukaguzi nchini hairidhishi kwani ni takribani 40% tu ya taasisi za elimu ndizo hukaguliwa kwa mwaka..
Juu ya uwezo wa wahitimu kujiajiri,
Ndugu Wananchi lengo kubwa la mfumo wowote wa elimu duniani ni kuzalisha rasilimali watu. Pamoja na Sera hii mpya kuzungumzia kwa ujumla kuwa itaweka utaratibu utakaowawezesha wahitimu kuwa na uwezo wa kushindana katika soko la ajira pamoja na kujiajiri; haitoi mwongozo ni kwa namna gani au hasa ni nini kitafanyika ili kuhakikisha lengo hilo linafanikiwa.
Changamoto kubwa ya zao la rasilimali watu linalozalishwa na shule na taasisi zetu imekuwa ni uwezo hafifu. Ushindani katika soko la ajira umeiweka pembeni Tanzania kiasi kwamba katika kushindania kazi za kimataifa tunashindwa kufua dafu hata mbele ya wenzetu wa Afrika Mashariki mathalani kutoka Kenya, Uganda na hata Rwanda. Ripoti ya World Economic Forum Network Readiness Index (2012 inaonesha kuwa Tanzania inashika nafasi ya mwisho miongoni mwa nchi za ukanda wa Afrika mashariki kwa kuwaandaa wananchi wake kuwa rasilimali watu yenye ujuzi na maarifa bora. Sera kama mwongozo ilipaswa kutoa utaratibu wa jinsi ya kulikabiri tatizo hili la uwezo wa wahitimu ili kuwezesha kuwa na ujuzi na maarifa yatakayowafanya waweze kuajiriwa na kujiajiri kirahisi zaidi.
Kuhusu lugha ya kufundishia
Ndugu Wananchi; Sera Mpya imeruhusu lugha za Kiswahili na Kiingereza kutumika kama lugha za kufundishia katika ngazi zote za elimu nchini. Tamko hili la kisera si tu ni ishara ya Taifa kutokuwa na msimamo juu ya lugha ya kufundishia and kujifunzia, lakini pia sera haijabainisha malengo mahsusi ya kutumia lugha mbili kufundishia katika ngazi zote za elimu . Uchaguzi wa lugha ya kufundishia lazima ulenge kuwawezesha wanafunzi kufundishwa na kujifunza ipasavyo ili kupata ujuzi na maarifa tarajiwa. Pia uchaguzi wa lugha ya kufundishia lazima ulenge kuwawezesha wahitimu wa kada mbalimbali za utaalamu kuweza kushindana katika soko la kitaifa na kimataifa Tunaishauri serikali kutathmini utekelezaji wa agizo hili la kutumia lugha mbili ikizingatiwa mambo mawili (a) urahisi wa upatikanaji wa maarifa ya mjifunzaji yanayokidhi soko la ajira na mwingiliano wa kijamii kati ya nchi na nchi.
Suala la usawa katika utoaji elimu,
Ndugu Wananchii; Pamoja na kuwa sera imetamka kuwa itahakikisha usawa katika elimu inayotolewa, bado haikueleza ni kwa namna gani hilo linaweza kufanikiwa wakati bado shule za umma zinakabiliwa na changamoto nyingi za mazingira ya kujifunzia na kufundishia ukilinganisha na shule binafsi.
Wakati wanafunzi katika shule za umma wakikosa walimu bora kutokana na walimu kukimbia malipo duni na mazingira magumu, wakikosa vitabu na maabara, wenzao katika shule binafsi wananufaika na mazingira mazuri, hamasa ya walimu, uwepo wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia na hivyo kuwawezesha kufanya wafaulu vizuri katika masomo yao kuliko wanafuzni wa shule za umma.
Kwa kushindwa kushughulikia suala hili, sera imeshindwa kupendekeza mbinu za kuondoa matabaka ya kielimu nchini ambayo yanawagawa watoto wa masikini kusoma kwenye shule zenye mazingira duni ya kufundishia na kujifunzia na watoto wa wenye uwezo kusoma katika shule zenye mazingira mazuri. Ikumbukwe kuwa wanafunzi walioko kwenye shule za umma ni asilimia 94.7 ya wanafunzi wote walioko elimumsingi kwa takwimu za mwaka wa 2015.
Rai yetu ni kuwa, ili kuleta usawa katika ujifunzaji ni lazima serikali ikishirikiana na wadau wa elimu iboreshe mazingira ya kufundishia na kujifunzia katika shule za umma. Sera itoe mwongozo juu ya viwango maalumu vinavyohitajika kabla shule yeyote haijasajiliwa ili kuanza kutoa huduma elimu kama inavyofanya kwenye shule binafsi. Ni vyema pia viwango hivi vikahusisha kuwepo kwa miundombinu bora na ya kutosha vikiwamo nyumba za walimu, madarasa, vyoo, maji, maktaba, maabara na vifaa vyote muhimu vya kufundishia na kujifunzia.
Kuhusu ElimuMsingi bila Ada
Ndugu Wanahabari; Pamoja na kuwa wazo hili ni zuri na linaungwa mkono na wadau mbalimbali wa elimu ikiwamo HakiElimu, sera haikutoa utaratibu maalumu wa jinsi ambavyo tamko hili litafanikiwa. Serikali ni lazima ikumbuke kuwa kuwaweka shuleni watoto na wakajifunza ipasavyo kunahitaji gharama, tumeshuhudia utekelezaji wa sera ya elimu ya 1995 kupitia miradi ya MMEM na MMES ikishindwa kutokana uhaba wa bajeti.
Tayari serikali imeanza kutekeleza mpango wa kutoa elimu bila malipo kwa kuondoa ada na michango. Japo serikali imedhamiria kutoa 100% ya fedha za ruzuku kwa ajili ya shughuli za uendeshaji wa shule, bado kuna changamoto ya namna gani serikali itasaidia uboreshaji wa miundombinu shuleni ikizingatiwa kuwa shule hazipati fedha za shughuli za maendeleo na zimekuwa zikitatua matatizo ya miundombinu kwa kutumia michango ya wazazi. Tayari suala la elimu bila malipo limeanza kuleta mkanganyiko kwa wazazi na walimu wakuu hasa kuhusu uchangiaji wa kuboresha miundombinu ambao bado haujawekwa bayana na serikali. Serikali haina budi kuandaa mkakati utakaowezesha utekelezaji wa elimu bila malipo huku ikilenga kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia katia shule zote za umma.
Ndugu Wanahabari; HakiElimu inapendekeza yafuatayo yawekwe kwenye miongozo ya utekelezaji wa Sera hii ili iweze kuleta tija na kusaidia kuboresha elimu yetu nchini.
Kama Taifa tunapaswa kutambua kuwa ulimwengu wa sasa wa sayansi na teknolojia unazifanya nchi na mataifa kuhusiana kwa karibu zaidi kuliko ilivyokuwa awali na hakuna taifa litakaloweza kuishi kama kisiwa. Ni muhimu Tanzania ikafanya tathmini hii na kuweka bayana msimamo wake kuhusu lugha tunayotaka kuitumia katika kuelimisha jamii na kizazi chetu kijacho. HakiElimu inaona kuwa njia pekee ya kutatua suala hili ni kuchagua lugha ambayo itaendana na uwekezaji ili kuwe na tija katika ufundishaji na ujifunzaji wa wanafunzi ili wanafunzi wapate maarifa na ujuzi stahili na kuweza kushindana katika masoko ya ajira kimataifa
Suala la umri na miaka ya mwanafunzi kukaa shuleni lisipewe uzito kiasi cha kusahau jukumu la msingi la elimu nchini ambalo ni kuelimisha na kupandikiza weledi kwa watoto wetu. HakiElimu tunapendekeza badala ya kuweka uzito katika umri wa mwanafunzi, ni vema ikaangalia zaidi nini mwanafunzi anajifunza na vipi kinamsaidia katika kukabiliana na changamoto za kimaisha.
Kwa kuwa Sera bado inaruhusu taasisi binafsi na wadau kushiriki katika utoaji elimu nchini, ni muhimu pia ikaweka utaratibu maalumu wa jinsi ambavyo shule za umma zitaboreshwa ili kuondoa tofauti ya shule za umma na binafsi na hivyo kuondoa matabaka kielimu.
Ubora wa elimu umekuwa ni changamoto ya muda mrefu sasa na ni muda muafaka kwa serikali kuandaa mikakati itakayowezesha kuboresha elimu yetu katika ngazi zote za elimu. Njia pekee ya kufanikisha hili ni kuwa na shule bora za umma ambazo zinahudumia wanafunzi wengi, kuwa na walimu bora na wenye hamasa ya kufundisha, kuwa na mifumo ya kufuatilia na kutathmini kiwango cha elimu katika ngazi zote na mifumo bora ya usimamizi wa shule.
Mwisho tunaipongeza Serikali kwa juhudi za kuhakikisha Sera ya Elimu na Mafunzo ya 2014 inapatikana.Hii ni baada ya kuwepo kilio cha muda mrefu kutoka kwa umma na wadau wa elimu kudai kufanyiwa marekebisho kwa sera za elimu za zamani ambazo ni dhahiri zilikwishapitwa na wakati na hivyo kushindwa kukabiliana na changamoto mpya za elimu.
Kupata nakala ya jarida lililobeba uchambuzi wa kina wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya 2014 tembelea http://www.hakielimu.org/publicatio...
Imetolewa na Idara ya Habari na Utetezi
HakiElimu
Mawasiliano: media@hakielimu.org

Friday, August 11, 2017


  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4

TEN/MET’s Meeting with Social Media stakeholders in Dar-es-salaam 2nd August 2017


TEN/MET's Meeting with Social Media stakeholders in Dar-es-salaam on 2nd August 2017 pic.twitter.com/UvbENNJ2Ou — Mtandao wa Elimu TZ (@ten_met) August 2, 2017 TEN/MET's Meeting with Social Media stakeholders in Dar-es-salaam 2nd August 2017https://t.co/5FLc3s9EHc pic.twitter.com/EBSl6Ksgut — Mtandao wa Elimu TZ (@ten_met) August 2, 2017 for more: https://khalfansaid.blogspot.com/search?updated-max=2017-08-02T04:18:00-07:00&max-results=7



Friday, August 11, 2017

Wakuu wa mikoa minne waanza kutekeleza agizo la Magufuli

By Burhani Yakub,Mwananchi byakub@mwananchi.co.tz



Kipindupindu chaanza kusambaa Mbeya




By Taboola