Tuesday, November 28, 2017

District councils unite for Gender Sensitive Budgets.

TGNP Mtandao hosted a two days experience sharing session with District chairpersons and mayors from Tarime, Ilala, Kishapu, Morogoro Rural and Mbeya districts as part of exchanging information and strategies on how to develop gender sensitive budgets.
As part of learning, TGNP Mtandao introduced the officials on various gender concepts and key areas that will be more potential when developing a gender sensitive budget, including water, health, agriculture and education.
Speaking during the session, Chairperson of Kishapu district, Mr Boniface Butondo explains on how gender budgeting has solved the problem of girls missing school during the menstruation days due to lack of facilities to cater them in schools such as Sanitary pads and clean water.
“ On our 2017/2018 budget we are fortunate to provide 30 Million as part of helping young girls who cannot afford sanitary pads in school, that has assisted them to attend school without missing, before we had this money, girls used to miss out 3 to 5 days because they lacked such facilities“ He explained.

 Chairperson of Kishapu district, Mr Boniface Butondo speaking during the session at TGNP Mtandao premises at Mabibo, Dsm
Recalling during the 2017 Gender festival, TGNP awarded the districts that managed to include the issue of sanitary pads to girls in schools that being Kishapu district and Kisarawe. This motivated various districts councils to take such step. This was proven by Mr Moses Misiwa Chairperson of Tarime District.
“ I am very excited attend this session, personally i was very inspired by my fellow district councils as we witnessed them awarded by the Vice president during the Gender Festival. As part of learning i would like to promise that this issue of sanitary pads will be included in our budgets, and am confident to say that we can afford that from our district revenues“ he says.
Apart from menstrual hygiene to girls in schools, the district chairpersons have also complained urging TGNP Mtandao to use the same force to address issues around agriculture. Recently the sector has been left behind by the government and it affects women who are the main actors.
Putting aside their political parties affiliations, the councils from the two districts agreed to set fund from internal sources to ensure that their budgets are very gender sensitive.
” we agree it is inevitable to develop if we are no being fair to some groups in the communities mostly women” they all say. 

Monday, November 27, 2017

Je unazijua siku 16 za kupinga ukatili wa Kijinsia?

Siku 16 za kupinga ukatili wa Kijinsia ni kampeni  ya Kimataifa  inayoongozwa na Kituo cha Kimataifa cha wanawake katika uongozi tangu mwaka 1991. Chimbuko la 16 za kupinga unyanyasaji wa kijinsia na mauaji ya kinyama ya kina dada wa Mirabelle yaliyofanyika nchini Dominica mwaka 1960. Mwaka 1991 Umoja wa Mataifa (UN) ulichagua Novemba 25 iwe siku ya Kimataifa ya Kupinga Ukatili wa Kijinsia ambapo kilele chake huadhimishwa Desemba 10 ya kila mwaka.
Siku hizi 16 hutoa mwanga wa uelewa kwa jamii kwa siku nyingine muhimu kama Novemba 29 ambapo ni siku ya Kimataifa ya watetezi wa haki za Wanawake , Desemba 1,Siku ya Ukimwi Duniani, Desemba 6 siku ya mauaji ya kikatili ya Montreal 1989 (wanawake 14 waliuawa na mtu aliyekuwa anawachukia wanawake) na Desemba 10 siku ya Haki za Binadamu Duniani.
Lengo la maadhimisho haya ni kutoa fursa kwa wanawake, wanaume,Vijana wa kike na kiume na wanaharakati wengine kukuza uelewa wa umma juu ya mchango wa wanawake katika maendeleo na kutafakari matokeo ya harakati za ukombozi wa mwanamke Kimapinduzi sambamba na kutafakari mafanikio hayo kwa miaka 20 ya tangu kuanzishwa kwa harakati hizo nchini mwaka 1993 TGNP ilipoanza.
Tutakumbuka kuwa maadhimisho haya huanza Novemba 25, ambayo ni siku ya Kimataifa ya Kupinga Ukatili dhidi ya Wanawake hadi Desemba 10 ambayo ni Siku ya Haki za Binadamu Ulimwenguni.  Siku hizi 16, TGNP na mashirika mengine yanayotetea haki, usawa wa Kijinsia na ulinzi dhidi ya makundi yaliyoko pambezoni hasa wanawake  wanaadhimisha kwa kufanya shughuli mbalimbali za kijamii, ikiwepo kusikiliza visa mkasa, kutoa shuhuda hadharani, kushirikina na mamlaka za kiserikali na dola latika kuunganisha nguvu kutokomeza kabisa Uakatili wa Kijinsia

Thursday, November 23, 2017

Vumilia,
Secondary scholar,
Tanzania

At just 13-years-old, Vumilia had supported herself through primary school, earning money collecting and selling firewood. But after completing primary school, she despaired in the knowledge that she could not progress to secondary school. Like many families, the cost of uniforms, books, shoes and school fees were beyond Vumilia’s parents’ means. And, to make matters worse, the nearest school was 10km away.  

Her grandmother said that Vumilia felt helpless, refusing to eat and crying every day. “She would ask me ‘Why is there no one to support me?’ I could only say, ‘You see how our life is. We cannot afford your school fees.’” All Vumilia could do was wait.
Before becoming a boarder, Vumilia started her 10 km walk to school at 4.30 a.m. every dayVumilia used to start her 10 km walk to school at 4.30 a.m. every day
Vumilia and her classmates complete forms identifying their school needs to CamfedVumilia and her classmates complete forms identifying their school needs to Camfed
After weeks of anxiety, and at her grandmother’s urging, Vumilia left home at 4:30 a.m. and began the long journey to secondary school. She had no uniform, no stationery, no pencils and no ability to pay her school fees. She had only the love of learning, and a hope that someone could help. When she arrived, she was crying and scared. Fortunately, the local secondary school is a Camfed partner school. Upon learning of Vumilia’s struggles, the head of the school provided her with a uniform, shoes and supplies from Camfed, allowing her to start school that very day. A week later, Vumilia was also invited to stay at the school’s makeshift dormitory space, where 140 other girls were also lodging to avoid long daily walks to school.
Upon learning that Vumilia would be supported through school, and would no longer have to endure the long daily walks, her grandmother was overjoyed. “We are very grateful,” she said. “She won’t live like this anymore.”

CHINA NA TANZANIA KUENDELEA KUSHIRIKIANA KATIKA SEKTA YA ELIMU.

Jamhuri ya Watu wa China imesema itaendela kuisaidia Tanzania katika sekta ya Elimu kwenye eneo la Elimu ya Juu, utoaji wa mafunzo ya Ufundi pamoja na kusaidia garama za uchapishaji wa vitabu vya masomo ya Sayansi kwa ajili ya shule za msingi na Sekondari.
Kauli hiyo imetolewa na Balozi wa wa Jamuhuri ya watu wa China Wang Ke wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako katika ofisi ndogo zilizopo jijini Dar es Saalam.
Katika mazungumzo yao Waziri Ndalichako amesema gharama za uchapaji wa Vitabu ni kubwa hivyo ni vyema Wizara ikawa na mitambo yake ya kuchapia vitabu ambayo itakuwa endelevu suala ambalo Balozi Wang Ke amekubaliana nalo na kuitaka Wizara kuandaa maombi ya mashine hiyo ili ubalozi uweze kufanyia kazi.
Jamhuri ya Watu wa China imesema itaendela kuisaidia Tanzania katika sekta ya Elimu kwenye eneo la Elimu ya Juu, utoaji wa mafunzo ya Ufundi pamoja na kusaidia garama za uchapishaji wa vitabu vya masomo ya Sayansi kwa ajili ya shule za msingi na Sekondari.
Kauli hiyo imetolewa na Balozi wa wa Jamuhuri ya watu wa China Wang Ke wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako katika ofisi ndogo zilizopo jijini Dar es Saalam.
Katika mazungumzo yao Waziri Ndalichako amesema gharama za uchapaji wa Vitabu ni kubwa hivyo ni vyema Wizara ikawa na mitambo yake ya kuchapia vitabu ambayo itakuwa endelevu suala ambalo Balozi Wang Ke amekubaliana nalo na kuitaka Wizara kuandaa maombi ya mashine hiyo ili ubalozi uweze kufanyia kazi.

UCHIMBAJI VISIMA HALMASHAURI YA NSIMBO

HALMASHAURI NCHINI ZA SHAURIWA KUBUNI VYA VIPYA VYA MAPATOI

Halmashauri nchini zimeshauriwa kubuni vyanzo vipya vya mapato ili ziweze kupata mapato ambayo yatasaidia katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo katika ngazi ya serikali za mitaa. Hayo yamesemwa Oktoba 27, 2017 mjini Dodoma na wawakilishi wa idara mbalimbali za Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) wakati wa mkutano uliojumuisha wanachama wa Policy Forum (PF) na maafisa wa OR-TAMISEMI.
Mkutano huo ulikuwa na lengo la kukutanisha wanachama wa PF na maafisa wa idara za OR-TAMISEMI kujadiliana namna ya kufanya kazi kwa pamoja hasa katika sekta ambazo zinaweza kuleta mabadiliko katika ngazi ya serikali za mitaa.
Mkutano huo ulitanguliwa na utambulisho wa pande zote mbili ambapo upande wa PF, Mwenyekiti wa Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa (LGWG), Kellen Mngoya alitoa usuli kuhusiana na mtandao wa PF na kazi zinazofanywa na vikundi kazi viwili ambavyo ni Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa (LGWG) na Kikundi Kazi cha Bajeti (BWG). Utambulisho wa OR-TAMISEMI ulitolewa na Sebastian Kitiku ambaye ni Mratibu wa Idara TAMISEMI.
Kitiku alianza kwa kutoa utangulizi wa jinsi ambavyo OR-TAMISEMI ilivyoalikwa kwenye mkutano wa wanachama wa PF wa  robo mwaka uliofanyika 2016 na kuomba wanachama wa PF kutumia maarifa na ujuzi wao katika kurahisisha miongozo iliyoandaliwa na OR-TAMISEMI kwa ajili ya matumizi katika ngazi za Serikali za Mitaa nchini.
Kitiku alipongeza juhudi zilizoonyeshwa na wanachama wa PF hasa wa kikundi kazi cha LGWG kwa kuweza kurahisisha miongozo hiyo kuwa katika lugha rahisi. Alitaja miongozo hiyo kuwa ni:
  • Mfumo wa Ruzuku ya Maendeleo ya Serikali za Mitaa: Mwongozo wa Ufuatiliaji na Tathmini;
  • Mfumo wa Ruzuku ya Maendeleo ya Serikali za Mitaa: Mwongozo wa Upimaji wa Mwaka na
  • Mfumo wa Ruzuku ya Maendeleo ya Serikali za Mitaa: Mwongozo wa Utekelezaji na Uendeshaji.
Wajumbe wa kikao hicho pia walipata nafasi ya kuweza kujadili suala la Serikali Kuu kuchukua baadhi ya vyanzo vya mapato vilivyokuwa vinakusanywa na Halmashauri. Akitolea ufafanuzi juu ya suala hilo Kitiku alieleza kuwa Serikali Kuu iliamua Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ikusanye kodi katika vyanzo vya mapato vya Serikali za Mitaa kwa kuwa ilionekana Halmashauri hazikuwa na mifumo madhubuti ya kukusanya mapato. Hata hivyo alieleza kuwa zoezi hilo ni la majaribio tu na linafanywa kwenye Halmashauri 30 ambazo ni kubwa ili kupima ufanisi katika ukusanyaji wa mapato.
Kitiku alieleza kuwa kwa sasa Serikali ina mpango wa kuboresha upelekaji wa fedha katika ngazi za Halmashauri. Mpango huo umeainishwa vyema katika vitabu vilivyoandaliwa na OR-TAMISEMI na kuandikwa kwa lugha rahisi na kikundi kazi cha PF na vitazinduliwa Oktoba 28, 2017 mjini Dodoma.
Wajumbe wa mkutano huo waliitimisha majadiliano kwa kukubaliana kuwa bado kuna umuhimu mkubwa wa kuwa na Hati ya Makubaliano (MoU) baina ya PF na OR-TAMISEMI. Pia OR-TAMISEMI iliiomba PF iwapatie watumishi wake mafunzo ya Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) ili waweze kutekeleza vyema shughuli zao za usimamizi wa utekelezaji wa SDGs katika ngazi za mikoa na mitaa.
Pia ilipendekezwa kuwa kikundi kazi cha LGWG kiwe kinashirikiana na Idara ya Serikali za Mitaa ya OR-TAMISEMI hasa katika kazi zinazohusiana na mafunzo kwa madiwani au uchambuzi wa sera mbalimbali zinazohusu Serikali za Mitaa, hili lilikuwa pia ni pendekezo litakalohitajika kuonekana kwenye Hati ya Makubaliano. Wajumbe walikubaliana pia kuwa wakati kikundi kazi cha LGWG kikiwa kinatembelea Halmashauri kiwe kinaenda na angalau afisa mmoja kutoka OR-TAMISEMI.